SUDANI KUSINI-USALAMA
Zaidi ya themanini waangamia katika makabiliano ya risasi Warrap, Sudan Kusini
Watu zaidi ya Themanini, wameuawa katika jimbo la Warrap nchini Sudan Kusini, baada ya kushuhudiwa kwa mapigano makali kati ya wanajeshi na raia wanaomiliki silaha.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mauaji haya yamethibitishwa na serikali jijini Juba na Umoja wa Mataifa, ambao umesema hali hii imetokea wakati jeshi lilipokuwa linawapokonya silaha raia wanaozimiliki kwa nguvu.
Ripoti zinasema, wanajeshi zaidi ya Hamsini wameuawa katika makabiliano hayo makali, ambayo yamekuwa yakishuhudiwa tangu mwishoni mwa wiki iliyopita.
Licha ya kuundwa kwa serikali ya pamoja, nchi ya Sudan Kusini imeendelea kushuhudia utovu wa usalama tangu mwaka 2013.