Odinga: Kenyatta acha kuitishia Mahakama Kuu
Kiongozi wa Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA, Raila Odinga amemtaka rais Uhuru Kenyatta kuacha kuitisha Mahakama ya Juu baada ya ushindi wao kufutwa wiki iliyopita.
Imechapishwa:
Akizungumza katika kampeni za siasa jijini Nairobi mwishoni mwa wiki kuelekea katika Uchaguzi mpya wa urais, Odinga amesema vitisho dhidi ya Mahakama na Jaji Mkuu Dvaid Maraga havikubaliki.
Hata hivyo, viongozi wa chama cha Jubilee wakiongozwa na Naibu rais William Ruto wameendelea kuikosoa Mahakama kwa uamuzi ambao wanasema ni kubadilisha uamuzi wa wananchi.
Mashirika ya kiraia nchini humo leo yanatarajiwa kuwa na kikao kulaani matamshi ya wanasiasa wa Jubilee dhidi ya Mahakama lakini pia kushinikiza kufanyiwa marekebisho ndani ya Tume ya Uchaguzi kabla ya uchaguzi mpya.