Pata taarifa kuu
KENYA-UCHAGUZI

Mahakama kusikiliza madai ya Odinga kupinga kuchaguliwa Kenyatta

Jumatatu hii Agosti 28 asubuhi Majaji saba wa mahakama ya juu nchini Kenya wataanza kusikiliza kesi ambayo kiongozi wa upinzani Raila Odinga anapinga kuchaguliwa tena kwa rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8, 2017.

Wafuasi wa Raila Odinga, wakati wa maandamano mbele ya Mahakama Kuu ya Kenya, Nairobi tarehe 18 Agosti 2017.
Wafuasi wa Raila Odinga, wakati wa maandamano mbele ya Mahakama Kuu ya Kenya, Nairobi tarehe 18 Agosti 2017. REUTERS/Baz Ratner
Matangazo ya kibiashara

Kesi hiyo ilianza siku ya Jumamosi kwa maelezo ya mwanzo ambayo kila upande ulitoa ili kuhakikisha nafasi kwa kusikilizwa rasmi.

Katika kikao cha kwanza ambacho kilichukua muda wa masaa matano, na kumalizika saa tano usiku,mawakili wa pande zote walitoa maombi yao  na matakwa yao ya kisheria.

Ombi kuu alilotoa James Orengo, mmoja wa mawakili wa Raila Odinga lilikuwa mahakama kumruhusu kumulikwa kwa mitambo ya kompyuta ambayo imehifadhi hati rasmi za uchgaguzi uliofanywa mapema mwezi huu.

Hata hivyo ombi la Orengo lilipingwa vikali na mawakili wanaomwakilisha rais Uhuru Kenyatta na pia tume inayosimamia uchaguzi Kenya.

Majaji wa mahakama hayo ya juu Kenya wanatarajiwa kutoa uamuzi wao saa nane leo mchana ikiwa watamruhusu ama kukataa ombi la wakili Orengo, kumulika kompyuta inayohifadhi hati za uchaguzi.

Hayo yakijri Mahakama ya juu nchini Kenya usiku wa Jumapili kuamkia lJumatatu hii imekubali kuingizwa kwa ushahidi kwenye kesi ya kupinga matokeo ya urais, hatua ambayo sasa imetenga uwanja wa makabiliano ya hoja kati ya mawakili wa rais Uhuru Kenyatta na wale wa kiongozi wa upinzani Raila Odinga.

Tofauti na ilivyokuwa mwaka 2013, majaji saba wa mahakama hiyo walitupilia mbali mapingamizi yaliyotolewa na mawakili wa pande zote mbili waliotaka kila mmoja ushahidi wake utupwe kwa sababu uliwasilishwa nje ya muda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.