Pata taarifa kuu
KENYA-UCHAGUZI

Kenyatta na Odinga wapiga kura

Wapiga kura zaidi ya milioni 19 nchini Kenya walipiga kura siku ya Jumanne kumchagua rais wao. Rais Uhuru Kenyatta na mpinzani wake mkuu Raila Odinga walipiga kura asubuhi.

Rais anayemaliza muda wake Uhuru Kenyatta, katika kituo cha kupigia kura cha Kiambu, katika Kaunti ya Gatund, Jumanne Agosti 8, 2017.
Rais anayemaliza muda wake Uhuru Kenyatta, katika kituo cha kupigia kura cha Kiambu, katika Kaunti ya Gatund, Jumanne Agosti 8, 2017. REUTERS/Baz Ratner
Matangazo ya kibiashara

Raila Odinga alipiga kura kwenye kituo cha Olimpiki kilichoko Kibera Kusini Magharibi mwa Nairobi.Uhuru Kenyatta alipiga kura katika kituo cha Mutomo, Kaskazini Magharibi mwa Nairobi.

Raila Odinga katika mkutano na waandishi wa habari usiku wa tarehe 8 kuamkia 9 Agosti 2017.
Raila Odinga katika mkutano na waandishi wa habari usiku wa tarehe 8 kuamkia 9 Agosti 2017. REUTERS/Thomas Mukoya

Kenyatta amekariri kuwa akishindwa uchaguzi atakubali matokeo.

Haya hapa ni mahojiano kati ya mwandishi wa RFI-Kiswahili James Shimanyula na rais anayemaliza muda wake Uhuru Kenyatta:

James: Rais habari ya asubuhi.

Uhuru Kenyatta: Salama habari yako

James: Kila la heri.

Uhuru Kenyatta: Asante sana twashukuru.

James: Unafikiria kwamba bado msimamo ni kwamba utapasua?

Uhuru Kenyatta: Msimamo ni huo huo tu.

James: Na umekubali kuwa utakubali matokeo?

Uhuru Kenyatta: Mimi nitakubali matokeo.

James: Rais Kenyatta tayari amewekewa kidole. Kuna wakati ambapo wasiwasi unakuzunguka kwa kichwa?

Uhuru Kenyatta: Ngoja nimalize na hawa tafadhali.

James: Tuko na wewe asante.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.