Vyama vya siasa vyaingia katika mchakato wa kutafuta wagombea Kenya
Vyama vyote vya siasa nchini Kenya vimeingia katika wiki muhimu ya kisiasa, kuwapata wagombea watakaopeperusha bendera ya vyama vyao wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Tayari chama cha ODM kinachoongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga, kimeanza mchakato huo katika kaunti mbalimbali.
Pamoja na hilo, vigogo wa muungano wa upinzani NASA, wanatarajiwa kukubaliana wiki hii kuhusu ni nani kati yao atakayepeperusha bendera ya upinzani dhidi ya rais Uhuru Kenyatta.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini humo Kadinali John Njue, ametoa wito kwa kampeni kufanyika kwa njia ya amani, na kuwataka vijana kutotumika kipindi hiki.