Pata taarifa kuu
KENYA-USALAMA

Watu kadhaa wauawa Mandera, Kenya

Watu waliojihami kwa silaha wameshambulia mtaa mmoja mjini Mandera, nchini Kenya. Watu kadhaa wanahofiwa kuwa wameuawa katika shambulizi hilo. Serikali inawatafuta waliohusika na mauaji hayo, lakini imewanyooshea kidole cha lawama wapiganaji wa Al Shabab.

Watu wawili, ambao walinusurika katika mashambulizi ya kundi la Al-Shabab yaliyosababisha vifo vya watu 36 katika eneo la Mandera, Desemba 6 mwaka 2014.
Watu wawili, ambao walinusurika katika mashambulizi ya kundi la Al-Shabab yaliyosababisha vifo vya watu 36 katika eneo la Mandera, Desemba 6 mwaka 2014. REUTERS/Goran Tomasevic
Matangazo ya kibiashara

Eneo la Mandera ilmekua likishambuliwa mara kwa mara na wapiganjai wa Al Shabab kutoka nchi jirani ya Somalia.

Mkuu wa jimbo la Mandera Ali Roba ameandika kwenye Twitter kwamba watu 6 wameuawa na mmoja kujeruhiwa. Lakini mashahidi wanasema idadi hiyo inaweza kuzidi kwani wanahofia kuwa watu zaidi ya kumi huenda waliuawa katika shambulizi hili.

Itakumbukwa kwamba wanajeshi wa Kenya wamekua wakitumwa nchini Somalia ili kuzima mashambulizi ya mara kwa mara nchini mwake na kuisaidia serikali dhaifu ya Somalia kuimarisha usalama nchini Somalia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.