Tanzania: Watu 22 wamefariki katika mgodi wa dhahabu
Nairobi – Watu 22 wamefariki dunia baada ya kuporomoka kwa vifusi vya udongo katika mgodi wa dhahabu wa Ikinabushu wilayani Bariadi mkoa wa Simiyu nchini Tanzania
Imechapishwa:
Ajali hiyo imetokea Alfajiri ya kuamkia Jumamosi ya januari 13 wakati wachimbaji wadogo wa dhahabu wakiendelea zoezi la uchimbaji.
Hali ilikuwaje kabla ya kuporomoka mgodi huo, Steven Masumbuko ni msimamizi wa mgodi huo.
“Udongo ulikuwa umezidiwa ndio ukawaponda watu. ” alisema Steven Masumbuko.
Steven Masumbuko
Kaimu kamanda wa jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Faustine Mtitu amesema mpaka sasa miili yote imeokolewa.
“Zoezi letu la uhakiki limetuonyesha kwamba hakuna mtu aliyesalia kwenye mgodi huu. ” alieleza Faustine Mtitu.
Faustine Mtitu
Serikali imechukua hatua gani kufuatia ajali hiyo, Anthony Mavunde ni Waziri wa Madini nchini humu.
“Kabla hawajaendelea na hali ilivyo kwa sasa, kwa sababu hali ilivyo kwa sasa, madhara yanaweza kutokea tena. ” alieleza Anthony Mavunde.
Anthony Mavunde
Mgodi huo umeporomoka zikiwa ni takribani siku tatu tangu uanze kazi ya uchumbaji, ukiwa ni mgodi wa pili wa dhahabu kuporomoka katika kipindi cha miaka minne katika mkoa huo.
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watu zaidi ya 21 kufuatia ajali ya kufunikwa na ardhi katika Mgodi wa Ng'alita, Wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu. Ndugu zetu hawa walikuwa wachimbaji wadogo katika eneo hili, wakijitafutia riziki zao, familia zao na kuchangia…
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) January 14, 2024
Steven Mumbi/ rfi Kiswahili/ Dar es salaam