Kenya na Iran zimetia saini mikataba ya ushirkiano na biashara
Nairobi – Rais William Ruto amesema kiwango cha biashara kati ya nchi hizo mbili bado kiko chini lakini kuna uwezekano wa kukua.
Imechapishwa:
Alieleza kuwa Kenya na Iran zitaweka utaratibu utakaowezesha mauzo ya nje chai, kahawa na nyama zaidi.
Kwa mujibu wa rais Ruto, hatua hii italeta uwiano wa kibiashara unaotarajiwa kati ya mataifa hayo mawili.
Kenya - Iran Media Briefing, State House, Nairobi. https://t.co/U5seR3nLHb
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) July 12, 2023
Rais Ruto pia ameeleza kwamba Kenya pia itatumia utajiri wa nchi hiyo ya Asia Magharibi katika teknolojia na uvumbuzi kwa maendeleo yake.
Alidokeza kwamba kuanzishwa kwa jumba la ubunifu na teknolojia la Iran mjini Nairobi kutatoa jukwaa mwafaka kwa biashara za Iran na Kenya.
At @StateHouseKenya, Nairobi, held bilateral talks with President Ebrahim Raisi where Iran agreed to boost Kenya’s pursuits in manufacturing, health and the blue economy through research and technology. pic.twitter.com/RWqMJClN7U
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) July 12, 2023
Mataifa hayo mawili yamepiga hatua katika masuala ya ushirikiano katika maendeleo, elimu, ufadhili wa masomo, miundombinu, afya, maji, uvuvi na kilimo.
Wakati wa mkutano wao, rais Ruto na Raisi walishuhudia kutiwa saini kwa makubaliano mapya katika nyanja za kilimo, mifugo, utamaduni na urithi, habari, teknolojia, uvuvi, makazi, maendeleo ya mijini na miji mikuu.
We also witnessed the signing of new MoUs and agreements in the areas of agriculture, livestock, culture and heritage, information, ICT, fisheries, housing, urban and metropolitan development that will further deepen our bilateral relations for sustainable growth. pic.twitter.com/UdKuDnG8QX
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) July 12, 2023
Rais Ruto amesifia uungwaji mkono wa Iran katika afya, akiitaja kuwa hatua muhimu kuelekea utimilifu wa huduma ya afya kwa wote nchini Kenya.
Naye rais Raisi alipongeza kujitolea kwa Kenya kuweka mazingira rafiki kwa biashara za kigeni.