Pata taarifa kuu

Kenya yakabiliwa na baa la njaa kutokana na ukame unaokumba Afrika Mashariki

Nchini Kenya, watu Milioni nne na laki tatu, wanakabiliwa na baada la njaa, kutokana na ukame unaoendelea kushuhudiwa, hasa katika maeneo ya Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo, kwa mujibu wa  ripoti ya pamoja na Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu, na Shirika la msalaba mwekundu nchini humo.

Punda akisubiri kubeba tanki la maji wakati wa utoaji maji unaoendeshwa na shirika lisilo la kiserikali la Save the Children huko Kubdisha mnamo Septemba 1, 2022.
Punda akisubiri kubeba tanki la maji wakati wa utoaji maji unaoendeshwa na shirika lisilo la kiserikali la Save the Children huko Kubdisha mnamo Septemba 1, 2022. AFP - YASUYOSHI CHIBA
Matangazo ya kibiashara

Ripoti hii inakuja, baada ya serikali ya Kenya  kuruhusu uzalishaji wa vyakula vinavytokana na mazao yaliyobadilishwa vinasaba maarufu kama GMO ili kusaidia kukabiliana na hali hiyo. 

Katika hatua nyingine, hatua ya serikali ya kuruhusu mazao ya GMO imepingwa vikali na wanaharakati likiwemo Shirika la Greenpeace Africa, kwa kuhofia usalama wa chakula hicho kiafya. 

Serikali jirani ya Tanzania nayo imesema haitaruhusu mazao hayo kuingia katika nchi yake kutoka nchini Kenya. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.