Pata taarifa kuu
UGANDA-RWANDA

Mwanasiasa wa Rwanda afukuzwa nchini Uganda

Uganda imesema imemfukuza nchini humo Robert Mukombozi mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda, ambaye chama chake cha Rwandan National Congress (RNC) kimepigwa marufuku.

 Rais wa Rwanda Paul Kagame, Kushoto, na mwenzake wa Uganda  Yoweri Museveni,  wakiwa pamoja katika siku zilizopita
Rais wa Rwanda Paul Kagame, Kushoto, na mwenzake wa Uganda Yoweri Museveni, wakiwa pamoja katika siku zilizopita AFP/File
Matangazo ya kibiashara

Hii imeonekana kama ishara ya Kampala na Kigali kuanza tena kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia ambao ulikuwa umeyumba miaka kadhaa iliyopita.

Aidha, hatua hii imekuja baada ya kuwepo kwa jitihada za kidiplomasia ambazo zimekuwa zikiongozwa  na mtoto wa rais wa Uganda  Yoweri Museveni, Jenerali Muhoozi Kainerugaba ambaye amekuwa akizuru jijini Kigali na kukutana na rais Paul Kagame.

Hatua hii ilisababisha kufunguliwa kwa mpaka wa Gatuna, uliokuwa umefungwa.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Kainerugaba ameandika kuwa, Mukombozi amefukuzwa Uganda kwa sababu yeye ni adui wa Rwanda na Uganda , na kuchapisha picha zake akielekea kuabiri ndege kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe.

Mukombozi, raia wa Rwanda, alizaliwa nchini Uganda, na amewahi kuwa mwanahabari kabla ya kwenda Rwanda, lakini baada ya kutofautiana na serikali, alikimbilia nchini Australia, kwa mujibu wa Habari za Kiinteljensia za nchi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.