Pata taarifa kuu
KENYA

Kenya yapokea dozi 880,000 ya Moderna kutoka Marekani

Kenya imepokea dozi 880,000 ya chanjo ya kuzuia Corona aina ya Moderna, kutoka serikali ya  Marekani, chini ya mpango wa Covax ,hii ikiwa mara ya kwanza kwa Moderna kutumika nchini humo.

Mwanamume huyu amesimama ndani ya duka lake jijini Nairobi wakati Rais Kenyatta akitoa hotuba mnamo Julai 2020, akitangaza hatua dhidi ya Covid-19.
Mwanamume huyu amesimama ndani ya duka lake jijini Nairobi wakati Rais Kenyatta akitoa hotuba mnamo Julai 2020, akitangaza hatua dhidi ya Covid-19. © AFP - Simon Maina
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa afya nchini Kenya Mutahi Kagwe ,amesema  chanjo hiyo ya Moderna, ni sehemu ya dozi milioni 1.7 ambazo zimetolewa na serikali ya Marekani, kupiga jeki kampeni ya uchomaji chanjo nchini Kenya, ambapo serikali inatazamia kuwachanja watu milioni 10 kufikia mwezi Desemba mwaka huu na wengine miloni 26 kufikia mwezi Juni mwaka ujao.

Aidha amesema dozi zingine karibu laki nne, chanjo aina ya Johnson and Johnson, zinatazamiwa kuwasili nchini juma hili.

Hadi Kenya imechanja asilimia mbili ya raia wake  kutumia chanjo ya AstraZenica na hii itakuwa ni mara ya kwanza Kenya itatumia aina nyingine ya chanjo.

 Kenya imeripoti maambukizi mapya 646 ndani ya siku moja iliyopita na vifo 30 katika kipindi hichi , hii ikifikisha idade yote ya watu walioambukizwa kufkia lakini mbili ,elfu ishirini mbili na tisa ,watu elfu nne mia nne na tisini na saba wakiwa wamepoteza maisha kutokana na Corona.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.