Pata taarifa kuu

China yarekodi visa vingi vya maambukizi ya virusi vya Uviko 19

China imeandikisha idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya Uviko 19  tangu kuzuka tena kwa maambukizi hayo mwezi Aprili, licha ya masharti mapya ya kukabiliana na janga hilo.

Sheria mpya ya walimu wa kigeni inaweza hatimaye kutishia maisha ya shule za kimataifa nchini China.
Sheria mpya ya walimu wa kigeni inaweza hatimaye kutishia maisha ya shule za kimataifa nchini China. STR / AFP
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema kwa muda was aa 24 zilizopita, watu 31,527 wameambukizwa. Mara ya mwisho kwa nchi hiyo kushuhudia idadi kubwa ya maambukizi kwa siku moja ilikuwa ni mwezi Aprili, ambapo watu Elfu 28 waliambukizwa. 

Maambukizi haya mapya yameanza kushuhudiwa katika jiji kuu Beijing na mji wa kibiashara wa Guangzhou. 

Hata hivyo, watalaam wa afya wanasema idadi hii ni ndogo kwa taifa hilo lenye watu Bilioni 1.4 na tangu kuzuka kwa ugonjwa huu ulioanzia nchini himo miaka miwili iliyopita, watu 5,200 ndio walippoteza maisha. 

China imekuja na sera ya kuhakikisha kuwa, kuna sifuri ya maambukizi ya virusi hivyo, hatua ambayo imesaidia kuokoa maisha ya watu, lakini imetatiza uchumi wa nchi hiyo ya bara Asia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.