Pata taarifa kuu

Mahakama ya Juu yakataa uamuzi wa Colorado unaomtangaza Trump kuwa hastahili

Mahakama ya Juu ya Marekani kwa kauli moja imebatilisha uamuzi wa mahakama ya Colorado Jumatatu iliyomtangaza Donald Trump kuwa hastahili katika kinyang'anyiro cha urais katika jimbo hili la kaskazini-magharibi kwa hatua yake wakati wa shambulio la Capitole.

Donald Trump, anayepewa nafasi kubwa ya kushinda katika kura za mchujo za chama cha Republican, mara moja alipongeza "Ushindi mkubwa kwa Amerika!!!", kwenye mtandao wake, Truth Social.
Donald Trump, anayepewa nafasi kubwa ya kushinda katika kura za mchujo za chama cha Republican, mara moja alipongeza "Ushindi mkubwa kwa Amerika!!!", kwenye mtandao wake, Truth Social. REUTERS - Jonathan Drake
Matangazo ya kibiashara

Uamuzi huu unakuja katika mkesha wa "Super Tuesday" ambapo majimbo 15, ikiwa ni pamoja na Colorado, hupanga kwa wakati mmoja kura zao za mchujo kwa uchaguzi wa urais mnamo Novemba. Bila kutaja hatua za rais anayemaliza muda wake wa Republican mnamo Januari 6, 2021, majaji hao tisa wanazingatia kuwa Bunge pekee na wala si Jimbo ndilo lililoidhinishwa kumwondoa mgombea kwenye kura ya uchaguzi wa urais.

Donald Trump, anayepewa nafasi kubwa ya kushinda katika kura za mchujo za chama cha Republican, mara moja alipongeza "Ushindi mkubwa kwa Amerika!!!", kwenye mtandao wake, Truth Social. Kati ya majimbo thelathini ambayo rufaa za kutostahiki zililetwa dhidi yake, ni mawili tu yaliyofaulu, huko Colorado, Maine (kaskazini mashariki), ambayo pia inapiga kura siku ya Jumanne, na Illinois (kaskazini). Mataifa kadhaa hata hivyo yalikuwa yakisubiri Mahakama ya Juu kutoa uamuzi wa mwisho.

Wachambuzi wa kisheria wamebishana juu ya uhalali na vile vile ufaafu wa kisiasa wa taratibu hizi. Lakini kila mtu amekubaliana na dhana kwamba mahakama yenye wingi wa wahafidhina, iliyokasirishwa na uamuzi wake wenye utata wa mwaka 2000 uliompa ushindi George W. Bush wa chama cha Republican dhidi ya Democrat Al Gore, ina nia ya kuepuka kuwa wazi kwa tuhuma za kuingiliwa.

Uamuzi huu ulitokana na Marekebisho ya 14 ya Katiba, yaliyopitishwa mnamo 1868, ambayo yalilenga wafuasi wa Shirikisho la Kusini lililoshindwa wakati wa Vita vya wenyewe kwa wenyewe (1861-1865). Haijumuishi katika shughuli za juu zaidi za umma mtu yeyote ambaye amejihusisha na vitendo vya "uasi" baada ya kula kiapo cha kutetea Katiba.

"Kwa sababu Katiba inaipa Congress, na sio Mjimbo, jukumu la kutekeleza Sehemu ya 3 (ya Marekebisho ya 14) dhidi ya wamiliki wa ofisi ya shirikisho na wagombeaji, tunabatilisha" uamuzi wa Colorado, unaelezea majaji tisa katika uamuzi wao wa pamoja.

Majaji watatu wanaoendelea kwa upande mmoja, na jaji mmoja wa kihafidhina, kwa upande mwingine, hata hivyo waliandika sababu tofauti kuunga mkono uamuzi wa Mahakama ya Juu. Hali ambayo haijawahi kushuhudiwa katika kesi hiyo ilitatanisha utabiri wowote, lakini wataalam wengi walihusisha majaribu ya majaji tisa kutafuta "penya" ya kuweka jina la Donald Trump kwenye kura.

Korti za Colorado zilizingatia kwamba hatua za Donald Trump mnamo Januari 6, 2021 ziliangukia katika Marekebisho ya 14. Siku hiyo, mamia ya wafuasi wa rais Donald Trump madarakani, wakiwa wamekasirishwa hasa na madai yake yasiyo na msingi ya udanganyifu katika uchaguzi, walivamia ^makao maku ya Bunge, Capitole, ili kujaribu kuzuia kuthibitishwa kwa ushindi wa mpinzani wake Joe Biden.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.