Pata taarifa kuu
KURA ZA MCHUJO

Uchaguzi wa urais Marekani: Trump anasema ana uhakika wa kushinda... kwa 'mara ya tatu'

Iowa ndipo zitazinduliwa kura za mchujo za chama cha Republican, na kwa hivyo kampeni za uchaguzi wa urais wa Marekani, zitaanza rasmi Januari 15, lakini Donald Trump ameamua kwenda katika jimbo hilo mapema, na kuandaa mikutano miwili wikendi hii. Jana, miaka mitatu baada ya shambulio la Capitol, rais huyo wa zamani alihakikisha kwamba atashinda tena, kwa "mara ya tatu".

Donald Trump alienda mapema Iowa, ambapo kura za mchujo za chama cha Republican ztaanza rasmi, na aliandaa mikutano miwili huko kwa mfululizo wikendi hii.
Donald Trump alienda mapema Iowa, ambapo kura za mchujo za chama cha Republican ztaanza rasmi, na aliandaa mikutano miwili huko kwa mfululizo wikendi hii. AP - Charlie Neibergall
Matangazo ya kibiashara

Na mwanahabari wetu nchini Marekani, Carrie Nooten

Huku mikutano yake miwili ikifuatana haraka, Donald Trump alitumia tena mbinu anayopenda zaidi: chukua nafasi kwanza, na kujiweke kwenye nafasi nzuri. Alijionyesha kama mshindi, na kufanya kura za maoni ambazo zimemuonyesha mshindi kwa miezi kadhaa. Na kisha, wakati wa hotuba ya saa mbili, alipuuzia tukio la kuzingirwa kwa Capitol, akitaja wavamizi wa makao makuu ya BungeJanuari 6 waliowekwa gerezani kama "mateka" wa serikali ya Marekani, alikosoa vyombo vya habari vinavyomtaja kama dikteta. Na zaidi ya yote, alimshambulia vikali Joe Biden, ambaye alimpa jina la utani "Joe tapeli".

"Kampeni ya hofu ya kutisha"

"Rekodi ya Biden," alisema, "ni safu isiyoweza kuvunjika ya udhaifu, uzembe, ufisadi na kutofaulu, zaidi ya hayo, anafanya vizuri (kicheko). Hii ndio sababu Joe tapeli aliandaa kampeni hii ya hofu ya kusikitisha."

Donald Trump pia anamshutumu mpinzani wake kwa kuipeleka nchi kwenye "vita vya tatu vya dunia", na kuongoza kampeni ya "tahadhari" dhidi yake, juu ya hatari ambayo aliiweka kwa demokrasia. Hatimaye, alikuwa na neno kwa ajili ya ulinzi dhidi ya Marekani, akisimulia jinsi alivyopindisha mkono wa Emmanuel Macron kwa kutishia kuongeza ushuru kwa uagizaji wa divai ya Ufaransa na champagne. Onyo ambalo nilinapaswa kuwatia wasiwasi viongozi wengi wa Ulaya.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.