UCHAGUZI-SIASA
Uchaguzi wa urais wa Comoro: Assoumani apita katika duru ya kwanza
Rais wa Comoro anayemaliza muda wake , Azali Assoumani, 65, ametangazwa mshindi siku ya Jumanne katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa urais uliyofanyika siku ya Jumapili katika visiwa vya Bahari ya Hindi, huku upinzani ukikashifu udanganyifu katika uchaguzi huo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mwanajeshi huyo wa zamani, ambaye atarejea kwa muhula wa tatu mfululizo, amepata 62.97% ya kura zilizopigwa, ametangaza mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, Idrissa Said Ben Ahmada Jumanne jioni.