Pata taarifa kuu
GHANA-USALAMA

Ghana: Zaidi ya kumi na sita waangamia katika mlipuko katika eneo la madini la Bogoso

Ghana inaomboleza vifo vya raia wake zaidi ya 16 waliofariki dunia katika mlipuko uliosababishwa na ajali baada ya gari kadhaa kugongana.

Katika eneo la tukio baada ya ajali ya barabarani iliyohusisha lori lililokuwa limebeea vilipuzi na gari nyine kadhaa, Januari 20 huko Apiate, karibu na Bogoso nchini Ghana.
Katika eneo la tukio baada ya ajali ya barabarani iliyohusisha lori lililokuwa limebeea vilipuzi na gari nyine kadhaa, Januari 20 huko Apiate, karibu na Bogoso nchini Ghana. AFP - ERIC YAW ADJEI
Matangazo ya kibiashara

Lori lililokuwa limebeba vilipuzi lililipuka baada ya ajali ya barabarani, Alhamisi, Januari 20, magharibi mwa nchi. Ripoti rasmi ya kwanza inabaini kwamba watu 17 wamefariki dunia na 59 kujeruhiwa, baadhi yao wakiwa katika hali mbaya.

Ripoti ya kwanza iliyotolewa na mamlaka ya Ghana unabaini kwamba ajali hiyo ilisababishwa na  lori lililojaa vilipuzi kugongana na magari mengine katika eneo la Apiate.

Mlipuko huo ulitokea mwendo wa saa sita mchana siku ya Alhamisi huko Apiate, sio mbali na Bogoso, mji wa kunakochimbwa madini ulioko kilomita 300 magharibi mwa Accra, mji mkuu.

Kulingana na picha za shirika la habari la AFP, ajali hiyo na mlipuko vimesababisha uharibifu mkubwa huku katika eneo la tukio kukionekana miili ya watu ambao hawakuweza kutambuliwakulinganana mashahidi.

Watu wakikagua uharibifu huo baada ya lori lililokuwa limebeba vilipuzi kugongana na pikipiki magharibi mwa Ghana na kusababisha mlipuko mkubwa uliosababisha vifo vya watu kadhaa na wengine kujeruhiwa. Ajali hiyo ilitokea Apiate, karibu na Bogoso, mji kunakochimbwa madini yapata kilomita 300 magharibi mwa Accra, mji mkuu wa nchi hii ya Afrika Magharibi.
Watu wakikagua uharibifu huo baada ya lori lililokuwa limebeba vilipuzi kugongana na pikipiki magharibi mwa Ghana na kusababisha mlipuko mkubwa uliosababisha vifo vya watu kadhaa na wengine kujeruhiwa. Ajali hiyo ilitokea Apiate, karibu na Bogoso, mji kunakochimbwa madini yapata kilomita 300 magharibi mwa Accra, mji mkuu wa nchi hii ya Afrika Magharibi. © Eric Yaw Adjei/ConnectFM/TV3 / AFP

Kwa mujibu wa ripoti ya kwanza ya uchunguzi, ni "ajali iliyohusisha lori lililokuwa likisafirisha vilipuzi kwa kampuni ya uchimbaji madini, pikipiki na gari la tatu iliyotokea karibu na transfoma ya umeme na kusababisha mlipuko huo," alisema Waziri wa Habari, Kojo Oppong-Nkrumah, katika taarifa iliyotolewa usiku wa Alhamisi kuamkia Ijumaa na kuripotiwa na shirika la habari la AFP.

Hospitali zote zilizo karibu na eneo la tukio zimewapokea majeruhi na kumeanzishwa mpango wa kuwahamisha walio katika hali mbaya hadi mji mkuu Accra.

Alhamisi alasiri, Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, alisikitishwa na "tukio baya, la kusikitisha na la kuhuzunisha" na kutoa rambirambi zake kwa familia za wahanga.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.