DRC-USALAMA
UN yahusisha makundi ya waasi na maafisa wa usalama kwa mauaji Mashariki mwa DRC
Umoja wa Mataifa unasema mauaji ya raia yanayoendelea kuripotiwa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, yanasababishwa na makundi ya waasi lakini pia maafisa wa usalama.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita, Tume ya Pamoja ya Haki za Binadamu katika Umoja huo inasema, raia 293 wakiwemo wanawake 63 na watoto 24 waliuawa.
Aidha, MONUSCO inasema kwa mwezi wa Agosti pekee, visa 739 vya ukiukwaji wa haki za binadamu viliripotiwa Mashariki mwa nchi hiyo, ikilinganishwa na 492 mwezi Julai.