Pata taarifa kuu
NIGER-CHAD

Niger yatangaza nia yake ya kushirikiana na Chad dhidi ya waasi wa FACT

Kulingana na jeshi la Chad, Idriss Déby inawezekana kuwa kifo chake kilitokana na majeraha aliyoyapata katika makabiliano kati ya vikosi vya jeshi la serikali na waasi wa FACT alipokuwa akiongoza mapigano Jumatatu Aprili 19.

Magari ya jeshi la Chad  yakionekana barabarani, wakati wapiganaji wa kundi lawaasi wa Front for Change and Concord in Chad (FACT) walionekana wakielekea mji mkuu kulingana na Marekani, huko N'djamena, Chad Aprili 19, 2021.
Magari ya jeshi la Chad yakionekana barabarani, wakati wapiganaji wa kundi lawaasi wa Front for Change and Concord in Chad (FACT) walionekana wakielekea mji mkuu kulingana na Marekani, huko N'djamena, Chad Aprili 19, 2021. REUTERS - STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Baraza la Kijeshi la Mpito, ambalo linakataa makubaliano yoyote au mazungumzo yoyote na kundi la waasi la FACT, linahakikisha kwamba waasi hao walikimbilia katika nchi jirani ya Niger na kuomba ushirikiano wa Niamey ili kuwaangamiza.

Kutoka chanzo rasmi nchini Niger, sasa inasemekana kuwa nchi hiyo inashirikiana kikamilifu na Chad. Kulingana na chanzo hicho, vikosi vya jeshi vya nchi hizo mbili  vinawasiliana vya kutosha. Baadhi ya watu wamekamatwa katika eneo la Darkou, bila hata hivyo kutaja idadi yao kwa wakati huu.

Siku ya Jumapili Aprili 25, msemaji wa Baraza la Jeshi la Mpito (CMT) alithibitisha kwamba waasi wa Front for Alternation and Concord in Chad (FACT) walisambaratishwa na vikosi vya jeshi vya Chad, na kwamba walikimbilia nchini Niger. Jenerali Azem Bermandoa Agouna alisema wako tayari kuwasaka, na aliomba ushirikiano wa Niger, na washirika wa G5 Sahel.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.