Pata taarifa kuu
NIGERIA-USALAMA

Kundi la waasi la Avengers latangaza kusitisha vita Nigeria

Nchini Nigeria kundi la waasi la Avengers, lililoendesha mashambulizi kadhaa dhidi ya mitambo ya mafuta na gesi katika eneo la Niger Delta, limesema Jumatatu hii kuwa limesitisha mapigano dhidi ya serikali ya Nigeria.

Wanajeshi wa Nigeria wakijianda kupiga doria usiku katika msitu wa Sambisa, katika eneo linalodhibitiwa na Boko Haram (Aprili 2014).
Wanajeshi wa Nigeria wakijianda kupiga doria usiku katika msitu wa Sambisa, katika eneo linalodhibitiwa na Boko Haram (Aprili 2014). © RFI/Ben Shemang
Matangazo ya kibiashara

Katika taarifa iliyorushwa kwenye tovuti yake, kundi hili, hata hivyo, linasema linasubiri kauli kutoka kwa Rais Muhammadu Buhari ya kupanga upya na kuruhusu kila jimbo kujitawala.

"Wiki moja iliyopita, kundi la waasi la Avengers lilitangaza nia yake ya kuweka chini silaha na kuanza mazungumzo na serikali.

Mashambulizi yaliyokua yakiendeshwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu na kundi hili ambalo linadai ugawaji sawa wa utajiri limedhoofisha uzalishaji wa mafuta nchini Nigeria, nchi ya kwanza barani Afrika kwa kuuza nje mafuta, ambapo kwa siku inauza mapipa 700,000.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.