Pata taarifa kuu

Mkuu wa AU ameelani shambulio la bomu katika kambi ya wakimbizi DRC

Rais wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat amelaani shambulio la bomu katika kambi za wakimbizi katika mji wa Goma Mashariki mwa DRC.

Umoja wa Afrika unataka makubaliano ya Luanda Angola kuhusu kusitishwa kwa mapigano mashariki ya DRC kuheshimiwa.
Umoja wa Afrika unataka makubaliano ya Luanda Angola kuhusu kusitishwa kwa mapigano mashariki ya DRC kuheshimiwa. AP - Moses Sawasawa
Matangazo ya kibiashara

Watu zaidi ya kumi waliripotiwa kuuawa katika shambulio la waasi wa M23 katika kambi ya Mugunda inayotoa hifadhi kwa watu waliopoteza makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya waasi hao na jeshi la seikali.

Miongoni mwa waliouawa kwenye shambulio hilo baya ni pamoja na wanawake na watoto, kitendo ambacho kimeendelea kukashifiwa.

Katika taarifa yake, Rais wa Tume ya AU Moussa Faki Mahamat ametuma pole zake kwa waathiriwa na shambulio hilo na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Adiha Moussa Faki ameeleza kusikitishwa na kuongezeka kwa mapigano na utovu wa usalama mashariki wa DRC, eneo ambalo kwa muda sasa limekuwa likikabiliwa na vita.

Waasi wa M23 wamekuwa wakituhumiwa kutekeleza mashambulio dhidi ya raia mashariki wa DRC.
Waasi wa M23 wamekuwa wakituhumiwa kutekeleza mashambulio dhidi ya raia mashariki wa DRC. AP - Moses Sawasawa

AU aidha imesema machafuko yanayoendelea kwa sasa ni kinyume na makubaliano ya mjini Luanda nchini Angola ya Machi tarehe 21 mwaka huu ambayo yalitaka kusitishwa kwa mapigano.

Soma piaDRC : EU yalaani shambulio la bomu kwenye kambi ya wakimbizi mjini Goma

Mwenyekiti wa Tume hiyo vilevile amesisitizia msimamo wa Umoja wa Afrika wa kuunga mkono suluhisho la kina la kisiasa kwa suala la amani katika eneo hilo.

Watu zaidi ya 10 waliuawa na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa katika shambulio hilo.
Watu zaidi ya 10 waliuawa na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa katika shambulio hilo. AP - Moses Sawasawa

Vilevile Faki amethibitisha kuunga mkono mchakato wa Luanda na Nairobi katika kutafuta amani ya kudumu mashariki mwa DRC na pia katika eneo lote la Maziwa Makuu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.