ZAMBIA
Edgar Lungu aongoza katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa raisi Zambia
Matokeo ya uchaguzi yanaendelea kutolewa nchini Zambia ambapo Rais Edgar Lungu anaongoza akifuatiwa na mpinzani wake wa karibu Hakainde Hichilema.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Matokeo kamili yanatarajiwa leo jumapili ambapo hadi sasa majimbo zaidi ya ishirini kati ya 156 yametangaza matokeo.
Hapo jana waangalizi wa uchaguzi walitoa wito wa utulivu kudumishwa baada ya madai ya ucheleweshwaji wa matokeo.
Tume ya taifa ya uchaguzi ilikanusha tuhuma kutoka kwa mgombea wa upinzani Hichilema, kwamba tume hiyo inashirikiana na chama tawala kuchelewesha matokeo.