Pata taarifa kuu
KENYA-Usalam

Kenya: wanajeshi wawili wauawa

Nchini Kenya wanajeshi wawili wa nchi hiyo wamepoteza maisha baada ya msafara wao kushmabuliwa na watu wanaominiwa kuwa wa kundi la Kigaidi la Al Shabab katika eneo la Lamu karibu na mpaka wa nchi hizo mbili. Wakuu wa usalama nchini Kenya wamekubaliana na Mahakama kupambana na ugaidi.

Shambulio liliyotokea katika kanisa moja mjini Mombasa.
Shambulio liliyotokea katika kanisa moja mjini Mombasa. Reuters/Joseph Okanga
Matangazo ya kibiashara

Hali ya usalama imekua ikidorora siku baada ya siku nchini Kenya, hususan katika miji ya Nairobi na Mombasa, miji inayo aminika kuwapa hifadhi raia wa wengi wa Somalia.

Polisi ya Kenya inaimarisha ulinzi eneo kulikotokea shambulio.
Polisi ya Kenya inaimarisha ulinzi eneo kulikotokea shambulio. REUTERS/Thomas Mukoya

Awali Serikali ya Kenya iliwataka raia kushirikiana na vyombo vya usalama ili kukabiliana na mashambulizi ya hapa na pale ambayo yanaendelea kushuhudiwa nchini Kenya. Serikali ilibaini kwamba itahakikisha usalama umezingatiwa nchini kote.

Raia wa Somalia waliofurushwa nchini Kenya wakiwasili kwenye uanja wa Mogadiscio, nchini Somalia, Aprili 9 mwaka 2014.
Raia wa Somalia waliofurushwa nchini Kenya wakiwasili kwenye uanja wa Mogadiscio, nchini Somalia, Aprili 9 mwaka 2014. REUTERS/Feisal Omar

Hivi karibuni polisi ya Kenya ilianzisha operesheni ya kupambana na makundi ya wanamgambo wa kislamu kutoka Somalia ambayo yanadaiwa kuendesha mashambulizi hayo. Polisi imekua ikiendesha msako dhidi ya raia Somalia ambao wanaendelea kuishi nchini humo kinyume cha sheria, na kuwarejesha makwao.

Kenya imekua ikishuhudia mashambulizi, baada ya kuwatuma wanajeshi wake nchini Somalia kujiunga na kikosi cha wanajeshi wa Umoja wa Afrika kinachosimamia amani nchini humo.

Mmoja kati ya waliyojeruhiwa katika mashambulizi yaliyotokea mjini Nairobi afikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Kenyatta mjini Nairobi Machi 31, 2014.
Mmoja kati ya waliyojeruhiwa katika mashambulizi yaliyotokea mjini Nairobi afikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Kenyatta mjini Nairobi Machi 31, 2014. REUTERS/Noor Khamis

Hivi karibuni kundi la al Shabab limetishia kuanzisha mashambulizi nchini Kenya.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.