Pata taarifa kuu
COLOMBIA-FARC

Mkataba wa amani kati ya serikali ya Colombia na FARC wapitishwa na Bunge

Mkataba wa amani uliosiniwa tena hivi karibuni kati ya serikali ya Colombia na kundi la waasi la FARC nchini Colombia, yalipitishwa na Bunge la nchi hiyo, Jumatano Novemba 30, siku moja baada ya kupitishwa na Baraza la Seneti.

Bunge na Baraza la Seneti vya Colombia vimepitisha pendekezo la Mkataba wa mani uliosainiwa hivi karibuni kati ya serikali ya Colombia na kundi la waasi la FARC.
Bunge na Baraza la Seneti vya Colombia vimepitisha pendekezo la Mkataba wa mani uliosainiwa hivi karibuni kati ya serikali ya Colombia na kundi la waasi la FARC. Reuters
Matangazo ya kibiashara

Colombia kuridhiwa Jumatano makubaliano ya amani na FARC, ambayo zamu maandishi umwagaji damu ukurasa zaidi ya nusu karne ya vita, lakini kwamba alikuwa kujadiliwa upya ni pamoja na mapendekezo ya upinzani baada ya kukataliwa na kura ya maoni mwezi Oktoba.

"Pendekezo la kupitishwa kwa mkataba wa amani limepitishwa," baraza la Wawakilishi lilitangaza, likisema kuwa pendekezo hilo lilipitishwa kwa kura 130 za wabunge wote walioshiriki kikao hicho, huku vifijo na nderemo vikipigwa katika jengo la Bunge.

Wabunge 130 walioshiriki kikao cha Bunge, kwa jumla ya wabunge 166, walipiga kura kwa kauli moja katika neema ya mkataba huo, unaopanga kupokonya silaha wapiganaji wa kundi la waasi la FARC na kukubaliwa kuwa chama cha kisiasa. Yote hayo yaliafikiwa baada ya karibu miaka minne ya mazungumzo kati ya serikali na kundi la wasi la FARC.

Rais Juan Manuel Santos, ambaye alitunukiwa wiki hiyo tuzo yaamani ya Nobel ka jitiohada zake za kumaliza vita, alikaribisha uamuzi huo wa Bunge na kuonyesha kuwa "Bunge limefanya kazi kubwa kwa tukio hilo la kihistoria kwa matumaini ya amani ya raia wa Colombia."

Toleo la kwanza la makubaliano hayo lenye kurasa 300, lilisainiwa Septemba 26, 2016 lilikataliwa Oktoba 2 katika kura ya maoni, ambapo kura ya "hapana" ilishinda na kuongoz kwa kura 50,000.

Wabunge kutoka chama kikuu cha upinzani cha CD cha mrengo wa kulia, kinachoongozwa na Seneta na Rais wa zamani Alvaro Uribe, walijiondoa katika kikao hichowakati wakupitishwa kwa pendekezo la mkataba huo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.