Pata taarifa kuu

Urusi yatekeleza mashambulio mazito ya anga dhidi ya Ukraine

Nairobi – Urusi ilitekeleza mashambulio makubwa ya anga dhidi ya Ukraine siku ya Ijuma, mashambulio ambayo yamesababisha karibia vifo vya watu 30 na kuwajeruhi mamia ya wengine.

Poland ilithibitisha kuwa kombora la Urusi lilipita katika anga yake.
Poland ilithibitisha kuwa kombora la Urusi lilipita katika anga yake. AP
Matangazo ya kibiashara

Haya ni mashambulio makubwa zaidi kuwahi tekelezwa na Urusi tangu ilipoivamia Ukraine karibia miaka miwili iliyopita. 

Shule, hosipitali ya kina mama kujifungua na majengo ya makazi ni miongoni mwa maeneo yalioharibiwa.

Mashambulio hayo ambabyo kombora la Urusi lilipitia anga ya Poland yalizua shutuma za kimataifa, washirika wa Kyiv wakitoa ahadi mpya za msaada wa kijeshi kwa Ukraine, ambayo imekuwa ikipambana na mashambulio ya wanajeshi wa Urusi tangu mwishoni mwa Februari 2022.

Ukraine imeendelea kuomba msaada zaidi wa kijeshi kutoka kwa washirika wake
Ukraine imeendelea kuomba msaada zaidi wa kijeshi kutoka kwa washirika wake REUTERS - VALENTYN OGIRENKO

Jeshi la Ukraine lilikadiria kuwa Urusi ilikuwa imerusha makombora 158 na ndege zisizo na rubani katika ardhi ya Kyiv, 114 kati ya hizo ziliharibiwa.

Umoja wa mataifa umelaani mashambulio hayo na na kutaka yakomeshwe mara moja.

Majengo ya kibiashara na yale ya makazi yameharibiwa katika shambulio hilo
Majengo ya kibiashara na yale ya makazi yameharibiwa katika shambulio hilo REUTERS - STRINGER

Poland ilithibitisha kuwa kombora la Urusi lilipita katika anga yake.

Msaidizi wa rais wa rais wa Ukraine Andriy Yermak baada ya mashambulio hayo ameeleza kuwa nchi yake inahitaji msaada zaidi kuzuia kile ametaja kuwa ugaidi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.