Uingereza kuendelea kusimama na Ukraine: David Cameron
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza David Cameron ambaye amefanya ziara jijini Kyiv na kukutana na rais Volodymyr Zelensky, ameahidi kuendeleza msaada wa kijeshi kwa Ukraine.
Imechapishwa:
Waziri mkuu huyo wa zamani amefanya ziara yake ya kwanza jijini Kyiv tangu ateuliwe kuhudumu katika wadhifa wa waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza.
London imekuwa mshirika wa karibu wa Ukraine tangu uvamizi wa Moscow ambapo pia imeendelea kuungana na mataifa mengine washirika wa Kyiv kutoa msaada wa kijesi nchini Ukraine.
Hosted @David_Cameron on his first visit to Ukraine as Foreign Secretary of the UK.
— Volodymyr Zelenskyy / Володимир Зеленський (@ZelenskyyUa) November 16, 2023
We had a good meeting focused on weapons for the frontline, strengthening air defense, and protecting our people and critical infrastructure.
I am grateful to the UK for its support!
🇺🇦🇬🇧 pic.twitter.com/zElLHsSaQT
Kwa mujibu wa Cameron, nchi yake itandelea kutoa msaada kwa Ukraine ikiwemo uungwaji mkono katika masuala ya kidiplomasia, kiuchumi na kijeshi mwaka huu na mwaka ujao.
Kwa upande wake rais Zelensky amemshukuru Cameron kwa kuikumbuka nchi yake wakati huu dunia nzima ikielekeza macho yake kuhusu kinachoendelea katika Mashariki ya kati.
Wizara ya nje ya Ukraine imesema waziri Cameron amefanya mazungumzo kuhusu masuala ya utengenezaji wa silaha na ulinzi katika bahari nyeusi.