Pata taarifa kuu

Silvio Berlusconi apongezwa mbali na kambi yake

Waziri Mkuu wa zamani wa Italia Silvio Berlusconi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 86 kutokana na saratani ya damu. Il Cavaliere, kama alivyopewa jina la utani, aliacha nyuma yake alama kubwa katika maisha ya kisiasa ya nchi yake, ambapo hatua zilivuka migawanyiko ya kisiasa. Nchini Ufaransa na pia kimataifa, mirengo mbalimbali, kushoto na kulia wamepongeza mtu mashuhuri katika historia ya Italia.

Silvio Berlusconi (katikati) akiwa na Giorgia Meloni, Rais wa sasa wa Baraza, na Matteo Salvini, huko Roma, Aprili 2018.
Silvio Berlusconi (katikati) akiwa na Giorgia Meloni, Rais wa sasa wa Baraza, na Matteo Salvini, huko Roma, Aprili 2018. AP - Gregorio Borgia
Matangazo ya kibiashara

Mazishi ya Silvio Berlusconi, aliyefariki Jumatatu Juni 12, akiwa na umri wa miaka 86, yatafanyika Jumatano hii katika kanisa kuu la mji aliozaliwa, Milan. Kwa ombi la familia ya Silvio Berlusconi - lakini pia ya Palazzo Chigi, Ofisi ya Baraza Kuu - mazishi ya Silvio Berlusconi yataadhimishwa kwenye Kanisa kuu la Milan. Itakuwa mazishi ya serikali. Mwili wa Rais wa zamani wa Baraza hilo umehamishiwa Villa San Martino, huko Arcore, kaskazini mashariki mwa Milan, alikoishi.

Mbele ya hospitali ya San Raffaele, ambapo rais wa zamani wa Baraza alifariki, mamia ya shada za maua yamewekwa. Shughuli zote za kisiasa za serikali ya Italia zimesitishwa tangu kutangazwa kwa kifo cha mwanzilishi wa Forza Italia, ambayo ni kusema kimo kinachowakilishwa na Berlusconi, ambaye chama chake ni mwanachama wa muungano wa serikali tawala. Nchini Italia, kila mtu anakubali kwamba ni sehemu ya Italia iliyoondoka asubuhi ya leo, hata kama wengi watakumbuka kwamba yeye pia ataingia katika historia kwa ajili ya kujitia mbali na vyombo vya sheria vya Italia, anaripoti mwandishi wetu huko Roma, Éric Sénanque.

Apumzike kwa amani.

Mkuu wa serikali ya Italia Giorgia Meloni alitoa pongezi kwa mshirika wake Silvio Berlusconi. "Silvio Berlusconi alikuwa mpiganaji zaidi ya yote. Alikuwa mtu ambaye haogopi kutetea imani yake na ilikuwa ni ujasiri wake na azimio lake ambalo lilimfanya kuwa mmoja wa watu mashuhuri zaidi katika historia ya Italia", amesema katika video iliyotumwa na baraza lake la mawaziri. "Berlusconi alikuwa kiongozi mkuu wa kisiasa ambaye aliashiria historia ya Jamhuri yetu", amesema Mkuu wa Nchi Sergio Mattarella katika taarifa, akimsifu "mtu wa ubinadamu mkubwa na mjasiriamali aliyefanikiwa".

Kwa upande wake, Matteo Salvini, kiongozi wa Ligi na Waziri wa Uchukuzi amepongeza ujasiri wa "Mtaliano mkubwa". "Moja ya bora zaidi wakati wote, kwa kila njia, kwa kila nyanja, isiyo na mpinzani," mwanasiasa huyo wa siasa kali za mrengo wa kulia ameandika kwene ukurasa wake wa Twitter. Pia alisikitika kumpoteza "rafiki mkubwa", akisema amehuzunishwa sana na kifo chake.

  Nchini Italia, hata wanasiasa wanaompinga Silvio Berlusconi wamepongeza mtu jasiri. "Silvio Berlusconi aliashiria historia ya nchi hii. Wengi walimpenda, wengi walimchukia: kila mtu leo ​​lazima atambue kwamba athari yake katika maisha ya kisiasa lakini pia kiuchumi, michezo na televisheni imekuwa isiyo na kifani, "aliandika Matteo Renzi, mmoja wa watu wenye nguvu kwa mrengo wa kushoto nchini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.