Uingereza : Boris Johnson kujiuzulu kama kiongozi wa chama cha Conservative
Waziri mkuu Boris Johnson anarajiwa kujiuzulu kama kiongozi wa chama tawala cha Conservative baadaye leo, lakini atandelea kuhudumu kama waziri hadi baadaye mwaka huu.
Imechapishwa:
Kiongozi mpya wa chama cha Conservative anatarajiwa kuchaguliwa na kuanza kuhudumu kama waziri mkuu kufikia mwisho wa mwezi Oktoba.
Hatua hii inajiri siku moja tu baada ya waziri mkuu Johnson kusisitiza kuwa hatajiuzulu kutokana na tuhuma ambazo zimekuwa zikimuandama.
Johnson alikuwa amewambia wabunge kwamba ataendelea kutekeleza majukumu yake, licha ya shinikizo za kumtaka ajiuzulu, kufutia kuongezeka kwa idadi ya mawaziri wanaojiuzulu na maafisa wengine wa serikali wanaomtuhumu Johnson kwa kukosa kuwachukulia hatua maafisa wa serikali yake wanaotuhumiwa kuhusika katika unyanyasaji wa kingono.