Pata taarifa kuu
UFARANSA-KAMPENI

Kampeni za uchaguzi wa kuwania kiti cha urais katika duru ya pili zaendelea Ufaransa

Nchini Ufaransa, rais Emmanuel Macron na Marine Le Pen wanaendeleza kampeni ya kusaka kura za kushinda urais, kuelekea duru ya pili Aprili 24.

 Wagombea wawili wa urais waendelea kunadi sera zao kuelekea duru ya pili ya uchaguzi wa urais.
Wagombea wawili wa urais waendelea kunadi sera zao kuelekea duru ya pili ya uchaguzi wa urais. REUTERS - BENOIT TESSIER
Matangazo ya kibiashara

Macron ambaye amepata uungwaji mkono wa rais wa zamani François Hollande,  leo amezuru Kanisa la Notre Dame jijini Paris, wakati huu pia akitoa mtazamo wake kuhusu mshahara mkubwa wa Mkurugenzi wa kampuni ya kutengeneza magari, Stellantis. 

Naye Marine Le Pen anaendeleza kampeni zake, Kusini mwa nchi hiyo na amesema iwapo ataingia madarakani ataitisha kura ya maoani kuhusu suala tata la wahamiaji. 

  Kura za maoni zinaonesha kuwa kutakuwa na ushindani mkali kati ya wawili hao lakini, Macron anatarajiwa kuibuka mshindi

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.