Ufaransa: Mjadala kuhusu kupitishwa kwa muswada wa chanjo wasitishwa bungeni
Wabunge wa Ufaransa walikuwa wakijadili Jumatatu, Januari 3, kuanzishwa kwa muswada wa sharia, utakaowataka watu nchini humo kuchanjwa ili kuruhusiwa kuingia katika maeneo ya umaa kama baa, Migahawa na mabasi yanayokwenda safari za mbali.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Kwa saa kadhaa, mashambulizi ya wabunge wa upinzani yaliongezeka dhidi ya Waziri wa Afya. Hata hivyo, kwa mshangao mkubwa, uchunguzi wa muswada huo ulisitishwa.
Ufaransa, moja ya nchi za Ulaya inaendelea kukabiliwa na kirusi cha Omicron na mpaka sasa watu zaidi ya Milioni tano hawajapata chanjo dhidi ya Civid 19.