Coronavirus: Idadi ya visa vya maambukizi yaongezeka Ujerumani
Idadi ya visa vipya vya maambukizi ya virusi vya Corona vilivyothibitishwa imeongezeka kwa visa 1,785 katika masaa 24 yaliyopita nchini Ujerumani, kulingana na takwimu iliyotolewa Jumanne na Chuo Kikuu cha Robert Koch (RKI).
Imechapishwa: Imehaririwa:
Ripoti iliyotolewa Jumatatu ilibaini visa vipya 1,775 vya maambukizi ya virusi vya Corona.
Jumla ya visa 143,457 vya maambukizi vimeripotiwa tangu kuzuka kwa janga la Covid-19 nchini Ujerumani.
Kuhusu idadi ya vifo vinavyotokana na virusi vya Corona, imeongezeka kutoka 194 jana Jumatatu hadi 4.598 leo Jumanne, kwa mujibu wa shirika la habri la Reuters.
Hata hivyo baadhi ya miji katika nchi zilizoathiriwa vibaya na janga la Corona barani Ulaya, ikiwa ni pamoja na Ujerumani, imeanza kufungua baadhi ya biashara na huduma, baada ya kuzifunga kwa muda tangu kuiingia kwa janga hilo barani humo.