Pata taarifa kuu
UFARANSA-UGAIDI-MAUAJI-USALAMA

Ufaransa: mshambuliaji wa tatu wa kujitoa mhanga atambuliwa

Karibu mwezi mmoja baada ya mashambulizi ya jijini Paris, Novemba 13, 2015, polisi hatimaye imemtambua mshambuliaji wa mwisho wa kujitoa mhanga ambaye alijilipua katika ukumbi wa Bataclan, karibu na eneo la Jamhuri. Ni mkazi wa Strasbourg, mwenye umri wa miaka 23, anayeitwa Mohamed Fouad Aggad.

Vijana wakiwasha mishumaa katika kumbukumbu ya wahanga wa mashambulizi ya Bataclan, Novemba 15 2015.
Vijana wakiwasha mishumaa katika kumbukumbu ya wahanga wa mashambulizi ya Bataclan, Novemba 15 2015. Reuters
Matangazo ya kibiashara

Kama yule ambaye aliyeandaa mashambulizi, raia wa Ubelgiji, Abdelhamid Abaaoud, Mohamed Fouad Aggad alikua aanajulina vema kwa sababu alijidhihirisha mwenyewe kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook akiweka picha yake alipokua nchini Syria, hasa ile yenye sifa mbaya akivaa kichwani utepe ambapo mbele ya utepe huo kulikua na bendera ya kundi la Islamic State.

Ni mtu ambaye alitambuliwa vema na licha ya hao aliweza pia kurudi Ufaransa bila hata hivyo Idara ya ujasusi kujua.

Mohamed Fouad Aggad alienda Syria na kaka yake na marafiki zake kumi kutoka eneo maarufu la Meinau alipokua akiishi katika mji wa Strasbourg mwishoni mwa mwezi 2013. Marafiki zake waliarudi mwezi Februari 2014, hasa baada ya kifo cha wenazo wawili katika mapambano na waasi wengine. Waliporudi walikamatwa.

Mohamed Fouad Aggad aaliamua kubaki nchini Syria. Taarifa za mwisho, zinabaini kwamba alikua akipigania nchini Iraq. Mke wake, mabaye ni raia wa Ufaransa, bado ypo Syria, na alijifungua hivi karibuni.

Ni mpiganaji wa sita wa kiislamu ambaye ametambuliwa baada ya kupoteza maisha katika mashambulizi mabaya kuwahi kutokea nchini Ufaransa kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.