GUINEA-UCHAGUZI-SIASA
Matokeo ya uchaguzi kutangazwa Ijumaa hii Guinea Conakry
Tume ya uchaguzi nchini Guinea Conakry imesema itatangaza matokeo ya awali ya uchaguzi wa serikali za mitaa hii leo ulioofanyika mwishoni mwa juma lililopita na kufuatiwa na vurugu ambapo watu zaidi ya 8 walipoteza maisha.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Watu zaidi ya hamsini wamekamatwa kuhusika ma matukio mbalimbali ya uhalifu wa baada ya uchaguzi huo ambao tume ya uchaguzi inalaumiwa kuchangia pakubwa.
Mkuu wa tume ya uchaguzi Salif Kebe amesema wako tayari kutangaza sehemu ya matokeo ya uchaguzi huo hii leo.
Hali ya utulivu imeendelea kushuhudiwa kwenye maeneo yaliyoshuhudia mapigano mwishoni mwa juma lililopita.