Pata taarifa kuu
GUINEA-SIASA

Dalein Diallo: Rais Conde atakiwa kuheshimu makubaliano na sio kupoteza muda

Upinzani nchini Guinea Conakry unaelekea kufaanikisha harakati za mageuzi nchini humo baada ya kufaulu kuandaa mihadhara ya wazi wakiitaka serikali ya nchi hiyo kutekeleza makubaliano yaliofikiwa kati ya vyama vinavyounga mkono utawala na upinzani mwaka 2016.

Waziri Mkuu wa zamani na mgombea wa uchaguzi wa urais nchini Guinea Conakry Cellou Dalein Diallo.
Waziri Mkuu wa zamani na mgombea wa uchaguzi wa urais nchini Guinea Conakry Cellou Dalein Diallo. REUTERS/Luc Gnago
Matangazo ya kibiashara

Makubaliano hayo yanaagiza kupitia upya sheria ya uchaguzi, ukaguzi wa dafatari la wapiga kura, kuandaa uchaguzi wa serikali za mitaa na kufidia familia za wahanga wa vurugu za kisiasa zilizotokea nchini humo katika miaka yta hivi karibuni.

Katika taarifa iliosainiwa na rais wa Guinea Alpha Conde amewataka washirika wake kutekeleza makubaliano hayo. Tibou Kamara ni waziri katika ikulu ya rais na mshahuri binafasi wa rais Alpha Conde.

Upande wake kiongozi mkuu wa upinzani Cellou Dalein Diallo ambae ametowa wito wa kuandamana Jumatano hii akidai kwamba rais Conde alitakiwa kuheshimu makubaliano na sio kupoteza muda.

Kiongozi wa upinzani Cellou Dalein Diallo hakiwa katikati ya waandamanaji katika mji wa Conakry, tarehe 14 Aprili.
Kiongozi wa upinzani Cellou Dalein Diallo hakiwa katikati ya waandamanaji katika mji wa Conakry, tarehe 14 Aprili. AFP PHOTO / CELLOU BINANI

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.