Pata taarifa kuu

Bunge la Libya lapiga kura dhidi ya serikali ya umoja wa kitaifa

Nchini Libya, Bunge la Libya lenye makao yake mjini Tobruk, lililokutana Jumatatu hii, Agosti 22, limepiga kura ya kutokua na imani na serikali ya umoja wa kitaifa (GNA), yenye makao yake mjini Tripoli na ambayo inaungwa mono na jumuiya ya kimataifa.

Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya,Fayez al-Sarraj, katika ofisi yake mjini Tripoli, tarehe 3 Juni 2016.
Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya,Fayez al-Sarraj, katika ofisi yake mjini Tripoli, tarehe 3 Juni 2016. REUTERS/Ismail Zitouny
Matangazo ya kibiashara

Pamoja na kura hii, Bunge limetoa wito kwa Baraza la Kirais kunda haraka serikali mpya.

Tangu Machi 29, tarehe ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa nchini Libya (GNA) kufuatia makubaliano ya kisaiasa baina ya wadau wote nchini Libya yaliyosainiwa nchini Morocco na kufadhiliwa na Umoja wa Mataifa Desemba 2015, ni mara ya kwanza Bunge, lenye makao yake mjini Tobruk, mashariki mwa Libya, kufanikiwa kukamilisha idadi ya wabunge inayohitajika kwa kuweza kukutana. Na hali hii ndio ilipelekea kura hii kupigwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatatu na Bunge, wabunge 101 walishiriki kikao hicho, kwa jumla ya wabunge 198. Aguila Saleh, Spika wa Bunge hilo mapoja na wabunge 61 walipiga kura dhidi ya serikali ya umoja wa kitaifaTripoli, mbunge mmoja alipiga kura katika neema ya serikali hiyo na wabunge 39 walijizuia kupiga kura.

Wabunge wengi wanaamini kwamba serikali ya umoja wa kitaifa (GNA) imeshindwa kutekeleza wajibu wake. Imenyesha "kutokuwa na uwezo wa kuongoza nchi," Mbunge Rida Omran amesema, kanla ya kuongeza kwamba serikali hii, "ambayo ni dhaifu toka iundwe," tayari imepoteza maafisa wake wanne.

Bunge limeomba Baraza la kirais, taasisi yenye wajumbe wanne, kuunda ndani ya siku kumi na tano, serikali mpya ya dharura itakayoundwa na mawaziri kati ya 8 na 12. Wakati huo huo, Bunge limesema kuwa maamuzi yote yaliyopitishwa na Baraza la kirais yanachukuliwa kama "batili".

Kwa mujibu wa tangazo la kikatiba lililotokana na makubaliano ya kisiasa ya Desemba 2015, Bunge lina kauli ya mwisho kwa kuonyesha imani yake kwa serikali.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.