AFCON 2024: Cameroon yaiburuza Gambia na kufuzu katika hatua ya 16 bora
Cameroon imeishinda Gambia (3-2) katika mechi kali na kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya Kombe la Afrika (AFCON) siku ya Jumanne huko Bouaké.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Simba wa Nyika walio na idadi sawa ya pointi (4) na tofauti ya mabao sawa na Guinea (-1) imemaliza ya pili kwa idadi ya mabao ya kufunga (5 dhidi ya 2). Gambia imeondolewa.
Karl Toko-Ekambi (katka dakika ya 56), James Gomez bao la kujifunga (katika dakika ya 87) na Christopher Wooh (katika dakika ya 90+1) walifungia Cameroon, dhidi ya mabao ya Ablie Jallow (katika dakika ya 72) na Ebrima Colley (katika dakika ya 85) waliofungia Gambia.