Pata taarifa kuu

Rasmus Hojlund amesajiliwa rasimi na Manchester United

Nairobi – Manchester United ilikamilisha usajili wa mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund kutoka Atalanta kwa ada ya pauni milioni 64 ($82 milioni) siku ya Jumamosi.

Mchezaji huyo amesajiliwa kwa kipindi cha miaka mitano
Mchezaji huyo amesajiliwa kwa kipindi cha miaka mitano © Manchester United
Matangazo ya kibiashara

Hojlund alikubali mkataba wa miaka mitano hii ikiwa ni mojawapo ya malengo ya  meneja wa United Erik ten Hag kumsajili mshambuliaji kabla ya kampeni mpya ya Ligi Kuu ya Uingereza kuanza.

"Sio siri kwamba nimekuwa shabiki wa klabu hii kubwa tangu nilipokuwa mdogo na nilikuwa na ndoto ya kuwa mchezaji wa Manchester United," Hojlund alisema.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 anaweza kuigharimu United pauni milioni 8 zaidi ikiwa vipengele vya nyongeza katika mkataba wake vitatimizwa.

Ten Hag alimfanya Hojlund kuwa mlengwa wake mkuu baada ya United kuripotiwa kukataa kulipa bei iliyotakiwa na Tottenham kwa mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, ambaye anaonekana kuwindwa na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich.

Rasmus Hojlund amesajiliwa kutoka klabu ya Atalanta
Rasmus Hojlund amesajiliwa kutoka klabu ya Atalanta © Manchester United

Mabingwa wa Ufaransa Paris Saint Germain walisemekana kuwa walikuwa wakiwinda saini ya Hojlund kabla ya United kushinda mbio hizo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.