Pata taarifa kuu

Riyad Mahrez na Henderson Kuhamia Saudi Arabia

Nairobi – Manchester City wamekubali kumuuza winga wao wa kulia Riyad Mahrez katika klabu ya Al-Ahli kwa ada ya pauni milioni 30.

Riyad Mahrez anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake kwenda nchini Saudi Arabia
Riyad Mahrez anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake kwenda nchini Saudi Arabia POOL/AFP
Matangazo ya kibiashara

Tayari mchezaji huyo wa kimataifa wa Algeria mwenye umri wa miaka 32 ameachiliwa na Manchester City wanaojiandaa kwa msimu mpya nchini Korea Kusini na Japan.

Klabu ya Al-Ahli yenye maskani yake Jeddah tayari imemsajili Roberto Firmino baada ya kumalizika kwa mkataba wake na Liverpool na kipa Edouard Mendy kutoka Chelsea katika msimu wa mbali.

Roberto Firmino amesajiliwa na Klabu ya Al-Ahli ya nchini Saudi Arabia
Roberto Firmino amesajiliwa na Klabu ya Al-Ahli ya nchini Saudi Arabia REUTERS/Andrew Yates

Mwananchi mwenzake Mahrez, Ryad Boudebouz alijiunga na Al-Ahli Septemba mwaka jana.

Mpinzani wa kihistoria wa Manchester, Liverpool, anajenga upya safu yake ya kiungo.

Msimu huu wa joto, The Reds walileta Alexis Mac Allister na Dominik Szoboszlai hili kuimarisha safu yao ya kati.

Jürgen Klopp anatazamiwa kupoteza kiungo mwingine muhimu wa timu yake ambaye ni Jordan Henderson.

Jordan Henderson anakaribia kuondoka kwenye kikosi hicho, kwani Liverpool wamefikia makubaliano na Al Ettifaq.

Jordan Henderson naye pia anatarajiwa kuondoka Liverpool
Jordan Henderson naye pia anatarajiwa kuondoka Liverpool POOL/AFP

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza anatazamiwa kusaini mkataba wa miaka 3 na klabu hiyo ya Saudia.

Henderson mwenye umri wa miaka 33, ambaye amesalia na miaka miwili kwenye mkataba wake Anfield, alikuwa Ujerumani na Liverpool kwa kambi yao lakini hakushiriki katika mchezo wao wa kwanza wa kujiandaa na msimu dhidi ya Karlsruher.

Pia alikosekana kiungo mwenza Fabinho, ambaye klabu hiyo ilipokea ofa ya pauni milioni 40 kutoka kwa Al-Ittihad siku ya Ijumaa.

Rangers manager Steven Gerrard has criticised the SPFL's handling of its end-of-season proposal
Rangers manager Steven Gerrard has criticised the SPFL's handling of its end-of-season proposal AFP/File

Nahodha wa zamani wa Liverpool Steven Gerrard aliteuliwa hivi karibuni kuwa meneja wa Al-Ettifaq jambo ambalo linachangia uhamisho mkubwa wa mastaa wa Liverpool.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.