Mason Mount amesajiliwa na Manchester United kutoka Chelsea
Nairobi – Manchester United imesajili kiungo wa kati wa Uingereza Mason Mount kutoka Chelsea kwa kima cha pauni milioni 55 .
Imechapishwa:
Mount, ambaye alikubali kandarasi ya miaka mitano na Manchester, alisema "hawezi subiri kuwa sehemu ya harakati za wachezaji wa United kushinda mataji makubwa" huko Old Trafford.
✍️ It's official.
— Manchester United (@ManUtd) July 5, 2023
Welcome to Manchester United, Mason Mount! 🔴#MUFC
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alihitimu kutoka akademi ya vijana ya Chelsea na kucheza mechi 129 za ligi kuu ya Uingereza, akifunga mabao 27.
Mason Mount will bring his midfield elegance to @ManUtd ✨ pic.twitter.com/N95k4PLmmf
— Premier League (@premierleague) July 5, 2023
"Si rahisi kamwe kuondoka katika klabu uliyokulia, lakini Manchester United itatoa changamoto mpya kwa awamu inayofuata ya maisha yangu," Mount alisema.
"Baada ya kushindana dhidi yao, najua jinsi kikosi ninachojiunga nacho kilivyo imara, na siwezi kusubiri kuwa sehemu ya mpango wa kikosi hiki kushinda mataji makubwa."