N'Golo Kante ni mchezaji wa Al-Ittihad ya Saudi Arabia
NAIROBI – Kiungo wa kati wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante amekubali kujiunga na mabingwa wa Saudi Arabia Al-Ittihad.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 nchini Uingereza katika klabu ya Chelsea, unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Juni mwaka huu.
Kante amekuwa akikabiliwa na majeraha na aliichezea Chelsea mechi tisa peke katika msimu wa 2022-23.
Kwa sasa mchezaji huyo ataungana na Karim Benzema katika klabu ya Al-Ittihad baada ya Mfaransa mwenzake kuondoka Real Madrid na kusaini mkataba wa miaka mitatu mwezi huu.
Hatua hiyo inahitimisha kipindi cha mafanikio makubwa katika soka la Uingereza kwa Kante.
Aliisaidia Leicester City kushinda ligi kuu ya Uingereza msimu wa 2015-16 kabla ya kuhamia Stamford Bridge. Akiwa Chelsea Kante alishinda klabu bingwa barani Ulaya, ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza, ligi ya Uropa na kombe la FA.
Aliteuliwa kuwa Mwanasoka Bora wa Chama cha Waandishi wa Soka na Mchezaji Bora wa Mwaka wa Chama cha Wachezaji Soka kwa 2016-17.
Farewell, N'Golo. Thanks for everything. 💙
— Chelsea FC (@ChelseaFC) June 21, 2023
Pia alitekeleza jukumu muhimu wakati Ufaransa iliposhinda Kombe la Dunia mnamo 2018.
Kante amesaini mkataba wa miaka mitatu na klabu hiyo wenye thamani ya £86m.