Pata taarifa kuu

Rais wa PSG Al-Khelaifi asifia viwango vya soka Afrika

NAIROBI – Na Paul Nzioki

 Nasser Al-Khelaifi, Rais wa PSG
Nasser Al-Khelaifi, Rais wa PSG AFP/File
Matangazo ya kibiashara

Rais wa klabu ya Paris Saint-Germain, Nasser al-Khelaifi,  amesisitiza dhamira yake katika soka la Afrika baada ya kushuhudia fainali kati ya Al Ahly ya Misri na Wydad ya Morocco katika kombe la klabu bingwa barani Afrika.

Al-Khelaifi ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Chama cha Vilabu Ulaya (ECA) ameongeza kusema kuwa kuna nia ya kuvipa vilabu vya Afrika rasilimali ndio viimarike zaidi.

Kocha wa PSG Christophe Galtier na rais wa klabu hiyo Nasser Al-Khelaifi.
Kocha wa PSG Christophe Galtier na rais wa klabu hiyo Nasser Al-Khelaifi. AP - Thomas Padilla

Katika mahojiano na beIN Sports, al-Khelaifi alipongeza mchezo  wa timu zote mbili na kuwataka watazamaji kutodharau kiwango cha soka barani Afrika.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyu ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa shirika la Habari la beIN, bara Afrika kwa muda mrefu limekuwa likijulikana kwa wachezaji wake mahiri na mechi za kusisimua zisizotabirika.

Rais huyo wa PSG alishuhudia mechi kati ya  Wydad na AI Ahly
Rais huyo wa PSG alishuhudia mechi kati ya Wydad na AI Ahly REUTERS - AMR ABDALLAH DALSH

"Tunathibitisha dhamira yetu ya kuipa soka la Afrika msaada unaohitajika ili kufikia uwezo wake kwa kuiwezesha kukuza vipaji vyake na kuipatia rasilimali muhimu," alisema na kuongeza kuwa soka sio tu kushinda ubingwa, bali pia kuinua ubinadamu kwa kiwango cha kimataifa.

"Leo, tunaendelea kuweka mipango ambao unapita zaidi ya jukumu la mpira wa miguu kwa maendeleo ya jamii zote ulimwenguni. Wakati wa Mkutano Mkuu uliopita wa ECA, tulichambua tu kile ambacho ECA inaweza kutimiza, na tunatazamia sura inayofuata. ECA ya siku zijazo itakuwa na ushawishi sio tu barani Ulaya, bali pia kote ulimwenguni, pamoja na Afrika.

Al-Khelaifi alimshukuru Fouzi Lekjaa, Rais wa Shirikisho la Soka la Kifalme la Morocco, na watu wa Morocco kwa ujumla kwa ukarimu wao, akiongeza kuwa umati huo wa watu wenye hamasa ulimvutia.

Al-Ahly walishinda ubingwa wa vilabu barani Afrika
Al-Ahly walishinda ubingwa wa vilabu barani Afrika © AFP - FADEL SENNA

Katika Fainali hiyo Al Ahly ilishinda ubingwa wake wa 11 karika ardhi ya Afrika na kuendeleza rekodi yake y akua klabu bora barani afrika mda wote kwa idadi ya mataji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.