Barkley na Pepe kuondoka katika klabu ya Nice
NAIROBI – Kiungo wa zamani wa Uingereza Ross Barkley ataondoka Nice mkataba wake utakapokamilika mwishoni mwa mwezi huu, klabu hiyo ya Ligue 1 imethibitisha.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Winga Nicolas Pepe, pia ataondoka Nice kama ilivyopangwa wakati mkataba wake wa mkopo wa mwaka mmoja kutoka kwa The Gunners utakapokamilika Juni 30.
Barkley, ambaye klabu zake za zamani ni Everton na Chelsea, alifunga mabao manne katika mechi 28 akiwa na Nice baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja miezi 12 iliyopita.
Beki wa pembeni Joe Bryan pia atarejea katika klabu ya Ligi ya Premia ya Fulham mkataba wake wa mkopo wa msimu mmoja utakapokamilika.