Pata taarifa kuu

Pochettino ndiye kocha mpya wa Chelsea

NAIROBI – Chelsea imemtangaza rasimi Mauricio Pochettino kuwa kocha wake mpya, kibarua anachokichukua wakati huu klabu hiyo ikiandikisha matokeo duni msimu uliopita.

Mauricio Pochettino, Kocha mpya wa Chelsea
Mauricio Pochettino, Kocha mpya wa Chelsea AP - Rui Vieira
Matangazo ya kibiashara

Pochettino amekubali kandarasi ya miaka miwili ambapo mkataba huo unaweza kuongezwa kwa mwaka mmoja kwa makubaliano ya pande hizo mbili.

Kocha huyo anarejea katika ligi kuu ya Uingereza miaka minne baadae baada ya kufutwa na mahasimu wa Chelsea jijini London Tottenham.

Pochettino mwenye umri wa miaka 51 hajakuwa na ajira tangu kutimuliwa na Paris Saint-Germain ya Ufaransa mwezi Julai mwaka wa 2022.

Kocha huyo anatarajiwa kuaanza majukumu rasimi tarehe moja ya mwezi Juali, akichukua nafasi ya Frank Lampard amabye amekuwa akiitumikia Chelsea kama kocha wa muda hadi kumalizika kwa msimu.

Lampard alikuwa meneja wa tatu wa Chelsea baada ya mmiliki wa klabu hiyo  Boehly kumtimua Thomas Tuchel mnamo Septemba na kisha kumfuta mrithi wake Graham Potter mwezi Aprili baada ya kipindi cha miezi saba.

Frank Lampard, aliyekuwa meneja wa muda wa Chelsea
Frank Lampard, aliyekuwa meneja wa muda wa Chelsea Reuters

Pochettino aliibuka kidedea baada ya Chelsea kufanya mazungumzo na meneja wa zamani wa Uhispania Luis Enrique na Julian Nagelsmann, ambaye alitimuliwa na Bayern Munich mwezi Machi.

Mauricio alikubali kuchukua mikoba ya kuinoa Chelsea mwezi Aprili, lakini uteuzi huo ukasitishwa hadi mwisho wa msimu.

Julian Nagelsmann alikuwa amepewa nafasi ya kuchukua majukumu ya kuinoa Chelsea
Julian Nagelsmann alikuwa amepewa nafasi ya kuchukua majukumu ya kuinoa Chelsea AP - Martin Meissner

Pochettino anakuja Stamford Bridge wakati huu ambapo The Blues wanakabiliwa na wakati mgumu ambapo wamemaliza katika nafasi ya 12 msiumu uliomalizika, nafasi wanayoshikilia tangu mwaka  wa 1996.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.