Rwanda: APR na Ryon Sports zinatafuta tiketi ya kucheza klabu bingwa Afrika
NAIROBI – Mwenyekiti wa Club ya APR Luteni Jenerali Mubaraka Muganga, akiongea na RFI, amesema timu yao ina mtihani mgumu wakati huu kufuatia wachezaji 4 katika safu ya ulinzi, wana majeraha.
Imechapishwa:
“Hatukufanya vizuri sana kama ilivyotarajiwa kwa sababu walinzi wetu watatu wamejeruhiwa.” amesema Mwenyekiti wa Club ya APR Luteni Jenerali Mubaraka Muganga
Mwenyekiti wa Club ya APR Luteni Jenerali Mubaraka Muganga
Kutotumia wageni katika club hii ya APR imekuwa changamoto wakati timu zingine zikiruhusiwa kutumia wachezaji watano.
Hii ikiwa sera ya timu hiyo ya kutotumia wageni hadi pale watakapotwaa ubingwa msimu huu.
Minani Hemedi ni Kiongozi wa mashabiki wa Kiyovu sports Club ametoa hamasa kwa mashabiki wake
“Lengo letu hasa tunachunguza mechi kwa mechi, tunakwenda kupambana na Sunarise, kwa bahati nzuri na sala za wanyarwanda, hili kombe tutalibeba.” amesema Minani Hemedi ni Kiongozi wa mashabiki wa Kiyovu sports Club
Minani Hemedi ni Kiongozi wa mashabiki wa Kiyovu sports Club
Kocha wa Gorilla FC Gatera Mussa ambaye, anatathmini kuhusu vigogo hao wanaoendelea kusaka taji la ubingwa.
“Labda timu ngumu ambayo APR imebaikia nayo ni AC Kigali bado mechi ya mwisho wanaweza wakateleza, kubeba ubingwa inakuwa ngumu.” amesema Kocha wa Gorilla FC Gatera Mussa.
Kocha wa Gorilla FC Gatera Mussa
Mpaka sasa Kiyovu wanaongoza ligi na alama 60, Apr wanashikilia nafasi ya 2 na alama 57 huku Rayon ikiwa kwenye nafasi ya tatu kwenye jedwari na alama 55.
Espoir FC ya Rusizi wao tayari wameshuka daraja la pili.
Timu bingwa wa ligi kuu huwakilisha Rwanda katika kombe la mabingwa barani (Africa CAF Champions League) wakati mabingwa wa kombe la Amani huwakilisha Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederaton Cup).