NBA: Golden State Warriors washinda taji la mchezo wa Kikapu
Klabu ya Golden State Warriors imeshinda taji la msimu huu la mchezo wa Kikapu kuwania ligi ya NBA nchini Marekani baada ya kuishinda Boston Celtics kwa vikapu 103 kwa 90.
Imechapishwa:
Hili ni taji la saba la NBA kwa klabu ya Golden State Warriors kutoka jiji la San Francisco.
Rais wa Rwanda Paul Kagame, kwenye ukurasa wake wa Twitter, amepongeza ushindi huo na kusema klabu yake imeshinda.
Washindi wa zamani
2022: Golden State Warriors
2021: Milwaukee Bucks
2020: Los Angeles Lakers
2019: Toronto Raptors
2018: Golden State Warriors
2017: Golden State Warriors
2016: Cleveland Cavaliers
2015: Golden State Warriors
2014: San Antonio Spurs
2013: Miami Heat