Bingwa wa mchezo wa Tennis duniani Ashleigh Barty astaafu
Bingwa nambari moja duniani katika mchezo wa Tennis kwa upande wa wanawake Ashleigh Barty ametangaza kustaafu.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Barty raia wa Australia mwenye umri wa miaka 25, ametoa tangazo hilo ambalo halikutarajiwa, akisema ametimiza ndoto yake katika mchezo huo na hana nguvu tena ya kuendelea.
Amechukua hatua hii baada ya kushinda taji la Australian Open, mashindano yalifanyika mwezi Januari.
FL𝑨𝑺𝑯 Barty⚡️@ashbarty | #AusOpenpic.twitter.com/EjzO9XBS60
— wta (@WTA) January 27, 2022
Kupitia mitandao yake ya kijamii, akionekana na rafiki yake na mchezaji mwenzake Casey Dellacqua, walioshirikiana katika mchezo huu, amesema muda wake wa kuachana na mchezo huo baada ya kushinda taji la Wimbledon mwaka 2021.
“Mafanikio kwangu ni kufahamu kuwa, nilitoa na kufanya nilichoweza.Nimeridhika.Nimefurahi, “ amesema.
“Sina tena nguvu za kuendelea, sina kingine cha kutoa au kuonesha,” ameongeza.
Mwaka 2019 alishinda taji la French Open na akafanya hivyo mwaka 2021 wakati aliponyakua ubingwa wa taji la Wimbledon, na kuwa miongoni mwa mataji 15 aliyoshinda baada ya kushiriki kwenye mashindano mbalimbali.