Pata taarifa kuu
MANCHESTER UNITED-SOKA

Kocha Ole Gunnar Solskjaer afutwa kazi na klabu ya Manchester United

Klabu ya soka ya Manchester United nchini Uingereza, imemfuta kazi kocha wake Ole Gunnar Solskjaer.

Aliyekuwa kocha wa  Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer.
Aliyekuwa kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer. Fabrice COFFRINI AFP/Archives
Matangazo ya kibiashara

Hii imekuja baada ya klabu hiyo kufungwa na Watford mabao 4-1 katika mechi ya ligi kuu ya soka nchini humo siku ya Jumamosi.

Nafasi yake sasa inachukuliwa kwa muda  na mchezaji wa zamani, Michael Carrick aliyewahi kuichezea klabu hiyo kati ya mwaka 2006 na 2018.

Kuondoka kwa Solskjaer raia wa Norway  hakujawashangaza mashabiki wa klabu hiyo na wapenzi wa kandanda dunia, kwa sababu ya matokeo mabaya ambayo Manchester United imekuwa ikiyapata.

Ameondoka Old Trafford wakati United ikiwa katika nafasi ya saba kwa alama 12. Kati ya mechi saba zilizopita za ligi kuu ya soka nchini humo, imepata ushindi mara moja tu kwa kuifunga Liverpool mabao 5-0.

Solskjaer, mwenye umri wa miaka 48, alimrithi Jose Mourinho kwa kipindi cha mpito  Desemba 2018 na baadaye kupewa mkataba wa kudumu mwezi Machi mwaka 2019 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Mwezi Julai mwaka huu, alikuwa amesaini   mkataba mwingine mpaka 2024.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.