BRAZILI-SOKA
Michuano ya Copa America kuanza Juni 13
Brazil imetajwa kuwa mwenyeji mpya wa mashindano ya mchezo wa soka, kuwania taji la Copa America, wiki mbili kabla ya kuanza kwa michuano hiyo iliyopangwa kuanza Juni 13.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Awali Argetina ndio iliyokuwa imepewa nafasi ya kuwa mwaandaji lakini kutokana na janga la virusi vya Corona nchini humo, ikapokonywa nafasi hiyo.
Mpaka sasa haijafahamika ni viwanja vipi vitatumika kuandaa michuano hiyo iwapo mashindano hayo yataendelea kwa sababu Brazil pia inakabiliwa na janga kubwa la Corona