Michuano ya kufuzu AFCON 2021 yatifua vumbi
Timu za taifa za mchezo wa soka za Nigeria, Namibia, Guinea-Bissau, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Malawi, zimeanza kwa ushindi, michuano ya kwanza, hatua ya makundi, kufuzu katika fainali ya mwaka 2021, kutafuta ubingwa wa Afrika nchini Cameroon.
Imechapishwa:
Wenyeji Cameroon hawakufungana na wageni Cape Verde, huku Lesotho wakilazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Sierra Leone, jijini Freetown.
Nigeria nao wakicheza nyumbani mjini Uyo, walitoka nyuma na kuwashinda jirani zao Benin mabao 2-1 katika mechi ya kundi L.
Jamhuri ya Kati nayo, iliifunga Burundi mabao 2-0 katika mechi ya kundi E.
Matokeo mengine:
Namibia 2-1 Chad (Kundi A)
Malawi 1-0 South Sudan (Kundi B)
Burkina Faso 0-0 Uganda (Kundi B)
Sudan 4-0 Sao Tome and Principe (Kundi C)
Angola 1-3 The Gambia (Kundi D)
CAR 2-0 Burundi (Kundi E)
Cameroon 0-0 Cape Verde (Kundi F)
Guinea Bissau 3-0 Eswatini (Kundi I)
Senegal 2-0 Congo (Kundi I)
Nigeria 2-1 Benin (Kundi L)
Sierra Leone 1-1 Lesotho (Kundi L)
Ratiba ya Alhamisi Novemba 14 2019:
Msumbuji vs Rwanda
Misri vs Kenya
Togo vs Comoros
Mali vs Guinea
Ghana vs Afrika Kusini
DRC vs Gabon
Algeria vs Zambia