Gor Mahia yafungiwa miaka miwili kushiriki michuano ya Cecafa
Gor Mahia imefungiwa kushiriki michuano ya Cecafa inayoandaliwa na shirikisho la Kandanda Afrika Mashariki na Kati, Cecafa kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu vilivyoonyeshwa na wachezaji wake.
Imechapishwa:
Gazeti la The Standard la Kenya, limearifu
Uamuzi huo,umefikiwa baada ya kikao cha kamati ya utendaji ya Cecafa kilichoketi Jijini Dar es Salaam baada ya timu hiyo kukataa kupokea zawadi ya mshindi wa tatu.
Pia Cecafa kupitia katibu mkuu Nicholaus Musonye, mbali naa kuipoka medali ya ushindi wa tatu pia Cecafa imeagizi shirikisho la soka Kenyaa kumchukulia hatua kocha wa Gor Mahia Dylan Kerr kutokana na matamshi yake machafu kwa waamuzi.