Pata taarifa kuu
HISPANIA-SOKA

Kocha wa Hispania ajiuzulu baada yaa kuhudumu kwa siku 25

Kocha Fernando Hierro aliyeiongoza Hispania katika fainali za Kombe la dunia amejiuzulu katika nafasi yake.

Aliyekuwa Kocha wa timu ya Taifa ya Hispania Fernando Hierro
Aliyekuwa Kocha wa timu ya Taifa ya Hispania Fernando Hierro REUTERS/Stringer
Matangazo ya kibiashara

Aidha ameachia ngazi kama mkurugenzi wa ufundi wa timu hiyo.

Hierro, mchezaji wa zamani wa Real Madrid na Timu ya Taifa ya Hispania alitangazwa meneja mpya siku mbili kabala ya kuanza kwa fainali za Kombe la dunia nchini Urusi baada ya kufutwa kazi kwa Julen Lopetegu ambaye alitangaza kuingia makubaliano yaa kuinoa Real Madrid baada ya fainali za kombe la dunia.

Licha ya kuongoza kundi B, Hispania, mabingwa wa mwaka 2010 Hispania ilifurushwa nje ya michuano hiyo na Urussi kwa changamoto ya mikwaju ya penati.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.